Search This Blog

Monday 24 May 2010

UAMUZI WA KUJITOA KWENYE SHINDANO LA MUZIKI BORA HAUTEKELEZEKI

Na Ibrahim Mkamba

NAOMBA nianze kwa kuwapongeza wasanii wote walioshiriki kwenye shindano la tuzo za Kili Music Awards mwaka huu. Ushiriki wa wasanii hao unaonesha ukomavu wao kisanii kwani walijua kulikuwa kuna kushinda na kushindwa.Kushinda,huongeza hamasa ya jitihada ya kwenda juu zaidi na kushindwa huongeza hamasa ya kufanya jitihada ili safari ijayo ushinde na kwenda juu zaidi.Pongezi za pekee ziwafikie wote walioshinda katika shindano hilo.

Kimsingi,huwa sielewi unakuwepo vipi uwezekano wa baadhi ya wasanii kujitoa kushiriki kwenye shindano hili.Uamuzi huo kisayansi hauwezekani kabisa hata kama wasanii hao wana hoja za msingi sana za kiuchumi na kijamii za kukataa kushirikishwa kwenye shindano hilo.Nitaeleza kwa nini hilo haliwezekani kisayansi lakini naomba nitangulie kuzungumzia kidogo maoni ya baadhi ya walioshuhudia onesho la mwana hip hop Mmarekani mwenye asili ya Jamaica,Sean Kingstone na wasanii wetu kadhaa kwamba Mmarekani huyo alifunikwa na wasanii wetu wa Bongo fleva walipotumbuiza kwenye sherehe ya kuwapongeza walioshinda tuzo za Kili Music Awards za mwaka huu ndani ya ukumbi wa Diamond Jubilee.

Sikuwepo siku hiyo lakini inawezekana kweli gwiji hilo la muziki la kimataifa lilifunikwa na vijana wetu kina Mwana FA,AY,Diamond, Cpwaa,Joh Makini na wengine kama ilivyoelezwa elezwa lakini naamini kufunikwa kwa mwanamuziki huyo mkubwa lakini mwenye umri mdogo, zaidi kulitokana na mazoea kwani kina AT na Stara Thomas, kwa mfano, walipoimba wimbo maarufu wa "Nipigie", wengi wa wabongo waliokuwemo ndani ya Diamond Jubilee walijua hicho ni kitu gani na wengi walikuwa wakifuatisha,bila kukosea hata kidogo,mashairi ya wimbo huo mzuri wanaoujua na kuupenda sana.

Sasa Kingstone akija na ngoma zake ambazo zinajulikana na wachache hapa kwetu,ni wazi wengi tusiozijua tulimuona si lolote lakini tutazithamini sana ngoma hizo zitakapokuja zoeleka masikioni mwetu kwa idadi kubwa.Hii ni kawaida hata kwa bendi zetu za muziki,wanamuziki wetu wa Bongo fleva, Modern Taarab na muziki wa bendi tunayoifahamu toka nje ya nchi. Toka kwao hao wote, nyimbo mpya tupu tusizozifahamu,zinapopigwa au kuimbwa nao kwenye onesho huwa tunaona tumeibiwa hata kama nyimbo hizo ni nzuri vipi.Huwa tunapenda kupata zile tunazozijua ambazo aghalabu huwa tunashiriki kuimba sanjari na wenye nyimbo zao wanapoziimba jukwaani.

Kwa mfano, vijana machachari toka Brazaville,Congo wa Extra Musica wakiwa na "full squad" ya kiongozi na mpiga solo mkali Roga Roga,rapa mahiri Kila Mbongo,mwimbaji mkali Oxy Oxygene,kina Ramatoulaye na wakali wote wa kundi hilo walikuja nchini mwaka 1998 kwa lengo la kutoa heshima kwa nchi hii ya kuzindulia hapa albam yao mpya ya "Etat Major" (E'ta Ma'ja) yenye wimbo huo mkali na kali sana nyingine za "La Pluine","Patinence","Ecart","Cri du Coeur","Racines" na nyingine zilizokuja kuwa maarufu sana hapa kwetu baadaye.

Licha ya umaarufu wa nyimbo hizo wa baadaye na baadhi yake mpaka sasa, siku ya kwanza walipojaribu kuzipiga kwenye uzinduzi wao hapa Dar es Salaam tulizipuuza mno kwani siku hiyo ya uzinduzi wa nyimbo hizo kila walipoanza kupiga wimbo wowote miongoni mwa nyimbo hizo,mashabiki wao wa bongo walipiga kelele kuwataka waache kupiga nyimbo wasizozijua.

Extra Musica walikwama kuzindua albam yao hiyo hapa.Ilibidi watupigie zile tu tulizozijua kama "Losambo","Fred Nelson","Success Extra","Kende",Angela" ,"Inondanation" na nyingine na kuufanya ukumbi wa Diamond Jubelee uchangamke sana.Kama wangekazania hizo za kuzindulia albam na kwa kuwa walishirikiana na Twanga Pepeta ya kina Adolph Mbinga na kina Banza Stone iliyokuwa na wimbo wa "Kisa cha Mpemba" na nyingine nzuri sana, mia kwa mia, tungeona Extra Musica wamefunikwa na Twanga.

Kwa hiyo ni hatari kuwajengea vijana wetu picha kwamba sasa wako juu ya watu kama Sean Kingstone wakati wana mambo mengi ya kujifunza toka kwao.Wakishaingiza imani hiyo vichwani ndiyo kujiona wako kileleni mwa mafanikio na matokeo yake kupotea kama kina Crazy GK,Suma G na wengine.Ndiyo,vijana wetu walikuwa na mengi ya kujifunza toka kwa Kingstone na watu wake kwa shughuli ya jukwaani lakini kubwa zaidi ninaloona walistahili kujifunza ni kila mtu kuthamini muziki wa nchi yake.

Nilisisimkwa mno na habari kwamba watu kadhaa wa kundi la Kingstone walichenguliwa ile mbaya na Taarab kiasi cha kuyarudi mangoma ya Taarab kwa nguvu na kununua baadhi ya CD zake.Unaona,hip hop yetu na R &B yetu kupitia Bongo fleva wala hawakuiona kwani waliiona kama igizo fulani lisilofanikiwa lakini mangoma ya Modern Taarab ya sasa, yasiyo tofauti na Msondo ya enzi ile, yaliwagusa sana.Kwa hiyo wana Bongo fleva wetu tukitaka tufanye biashara ya uhakika ya kimataifa tutumie kupitishia "mistari" yetu kwenye mapigo ya kikwetu kama yale ya Mzee Yussuf ya "Mchum,Issa Kijoti" au ya "Chaja ya Kobe" ya Babu Ayub jambo walilotufundisha kina Kingstone.

Tukirudi kwenye hoja ya msingi,kisayansi kwenye mashindano ambayo mshiriki wake huwa mashindanoni mara tu anaposhiriki kwenye shughuli ya kushindanishwa,hakuna uwezekano wa mtu kujitoa mashindanoni.Njia pekee ya kujitoa ni kutofanya shughuli hiyo kwa kipindi cha kushindanishwa.Kwa mfano,ligi kuu ya soka inapoanza tu inatajwa zawadi ya mfungaji bora.Sasa Mussa Hassan Mgosi, kwa mfano, hawezi kusema kwamba yeye amejitoa kwenye shindano la ufungaji bora wakati ni mchezaji na tena ni mshambuliaji na anacheza kwenye ligi hiyo.

Njia pekee ya yeye kujitoa kwenye shindano la mfungaji bora ni kutochezea klabu yoyote inayoshiriki ligi hiyo.Tena hana haja ya kutuambia kwamba hatashiriki shindano hilo kwani moja kwa moja atakuwa hayumo kama ilivyokuwa kwa watu kama Balozi Dola Sol,Mr Nice,Mandojo na Domokaya,Mabaga Fresh na wengine kwenye tuzo za Kili Awards za mwaka huu kutokana na kutofanya lolote la kimuziki kwenye mwaka huu ulioshindaniwa.

Kisayansi, kama ulifanya kazi ya muziki ndani ya kipindi cha mwaka 2009/2010,moja kwa moja umo shindanoni kwenye kuwania tuzo ya Kili Music Awards,utake usitake kwani tunaweza kuikubali kazi yako hata kama mwenyewe hauko tayari kupambanishwa na wengine.Kushindwa kwani kitu gani? Lazima awepo mshindi hata kama kazi zinazoshindanishwa ni nzuri tupu. Kwa mfano,kwangu binafsi utanipa wakati mgumu kuchagua wimbo bora wa waimbaji walioshirikiana baina ya "Nipigie","Njia Panda" na wimbo mpya unaokuja kasi sana wa "Wrong Number" (wimbo unaoelezea kiufasaha tatizo mojawapo la simu za mkononi miongoni mwa wanandoa).Pamoja na ubora wa kazi zote hizo tatu,zikishindanishwa lazima moja itashinda.Tujenge utamaduni wa kukubali matokea na hivyo kutoogopa kushindana.

Naomba wahusika wa tuzo za Kili Music Awards ifanyieni kazi changamoto yangu ili kila anayeshiriki kwenye masuala ya muziki ajue kuwa moja kwa moja ni mshiriki wa mashindano ya muziki ya kipindi husika kama Jerry Tegete anavyokuwemo kwenye shindano la mfungaji bora hata kabla ligi haijaanza kwa sababu tu yeye ni mshambuliaji na amesajiliwa kucheza kwenye ligi hiyo.Nitashangaa siku John Boko mshambuliaji wa timu ya ligi kuu atakapotangaza kuomba kuenguliwa kwenye shindano la ufungaji bora wa ligi kuu kama baadhi ya wanabongo fleva wetu wanavyofanya kwenye Kili Music Awards wakati muziki wao unasikika hewani mwaka mzima unaoshindaniwa.

Wednesday 5 May 2010

JANUARY 2010 MESSAGE TO CAF

Message to:-
info@cafonline.com
I am Ibrahim Jaffar Mkamba, Tanzanian by birth. On January 24th, 2010 I will be exactly 48 years old.
I would like to suggest that our Africa Cup of Nations finals, which are currently taking place in Angola, should be held in June of years with odd numbers. That is to say, if we start the suggested arrangement in the year 2013, subsequent finals will in succession take place in 2015,2017,2019,2021 onwards. That will be so if we cling to lapse of two years after every finals.
If we decide to make it four years, those finals should take place in 2013, 2017, 2021, 2025, 2029 and so on.
Reasons for my suggesting so are based on making African players, who largely are in European Club squads, play with large part of their thinking directed to those finals rather than the case is now whereby mostly they think of their career in Europe and hence to under perform in this competition.
Also, if our finals take place in years of odd numbers, it means we will have all of them do so in different years from those of Euro and World Cup.
I hope you will consider my suggestion positively because I believe it is practicable.

Ibrahim Jaffar Mkamba, Dar es Salaam, Tanzania

Thursday 29 April 2010

HAKUNA MTU MUHIMU KULIKO WOTE POPOTE PALE


Na Ibrahim Mkamba

KWA mujibu wa kamusi ya Kiingereza ya Longman toleo jipya,neno la Kiingereza "indispensable" lina maana ya tafsiri yangu isiyo rasmi ya mtu ambaye au kitu ambacho ni muhimu saaana kiasi cha utekelezaji kutowezekana bila ya kuwepo kwa mtu huyo au kitu hicho.Kwa sababu Kiswahili hakina neno moja la mtu huyo au kitu hicho,naomba nitumie zaidi neno la Kiingereza,"indispensable" kufikisha ujumbe wangu kwa Watanzania wenzangu.

Mtu kujenga picha kwa wengine kwamba yeye ni "indispensable" ni ugonjwa ambao umekuwa ukiathiri sana mipango yetu mingi muhimu.Timu kubwa ya soka ya nchi hii kama Yanga au Simba,ikikabiliwa na ugonjwa huo,uuzaji wa wachezaji nje unakuwa mgumu kwani kutajengeka imani kuwa Jerry Tegete,Mrisho Ngassa,Mussa Hassan Mgosi au Juma Kaseja ni "indispensable" kwenye timu kiasi cha kuuza wachezaji hao kutaathiri mafanikio ya timu.Huu ni upuuzi uliopitiliza kama nitakavyojadili baadaye.

Leo utasema mwanamuziki huyu hawezi kuruhusiwa kuhama bendi hii kwa sababu yeye ni "indispensable"! Kivipi? Kwani mtaalam wa idara anayoshughulikia Tanzania nzima ni yeye tu? Upuuzi mtupu!

Kimsingi,watu ambao wanajiaminisha kwa wengine kwamba wao ni "indispensable" ni wale wenye sifa za ubababishaji,kung'ang'ania nafasi wakati uwezo wao ni wa kuutilia shaka,wenye upeo mdogo sana na wenye akili zilizochoka kiasi kwamba hawawezi kubuni vitu vipya vya kuyafanya mambo yaende.

Watu hawa mara nyingi hupenda sifa zote za utekelezaji mzuri ziwe zao kwamba wao tu ndiyo waliofanikisha mazuri hayo na ikitokea lawama kiutekelezaji,mara zote hufanya juhudi za kuonyesha kwamba wao hawakuhusika kabisa na kosa hilo licha ya ukweli kwamba yote, mafanikio na kuteleza kiutendaji, yanatokea katika ofisi hiyo hiyo huku wao wakiwemo ofisini!

Moja ya athari kubwa,miongoni mwa nyingi za kuwa na watu wanaojiaminisha kuwa "indispensable" kwenye jumuiya yoyote ni kuwafanya wale wenye uwezo mkubwa kiakili kutotumia uwezo wao inavyopaswa kutokana na kubanwa na hao "indispensable" kama itakavyofafanuliwa baadaye.Matokeo ya hali hiyo ni kwa mipango ya maendeleo ya jumuiya hiyo kwenda chini. Mara nyingi hao wenye uwezo huangalia kwa masikitiko mambo yanavyopelekwa ovyo lakini wanachelea kueleza ukweli baada ya huko nyuma kuponea chupuchupu kufukuzwa jumuiyani kwa kurekebisha kosa la "indispensable" kwa nia ya kujenga.

Si mara zote watu hao hujinadi wenyewe kuwa "indispensable" bali mara kadhaa wanyonge miongoni mwetu huwatengenezea hali hiyo ambayo wao huikubali bila kutoa kauli bali kwa vitendo tu.Angalia,Yanga ikifanya vizuri,sifa zote kwa tajiri wao Yussuf Manji lakini ikiteleza,lawama zote kwa Mwenyekiti Iman Madega na safu yake ya uongozi! Simba ikifanya vizuri,sifa kwa "Friends of Simba" tu lakini ikiboronga,lawama kwa uongozi.Hata makocha hupewa ngazi ya kati kwenye yote mawili,mafanikio na kukosekana kwa mafanikio.

Utashangaa kitu kimoja,eti mtu anakuwa nje kiofisi,sehemu ya mbali na ilipo ofisi hiyo,yaani kona nyingine kabisa ya nchi.Mara linajitokeza suala la kutafutiwa ufumbuzi.Atakachofanya "indespensable" huyo ni kurudi ofisini haraka ili ashughulikie suala hilo! Cha kusikitisha,kutokana na upeo wake mdogo,anaweza kufika na kuvuruga mikakati mizuri iliyopangwa na kuanza kufanyiwa kazi na aliowaacha ofisini ambao akili zao zimejaa ubunifu mwingi.

Mambo yakianza kwenda ndivyo sivyo kutokana na muingilio wa kazi wa "indispensable" huyo asiye na chembe ya ubunifu,inabidi wale wenye ubunifu waachiwe waendelee na mipango yao waliyoibuni ya kuondoa kadhia hiyo.Mwisho mambo yanakaa vizuri na kitakachofuata ni kwa "indispensable" huyo kujinadi kwamba bila yeye kurudi toka alikokuwa,mambo yangeharibika vibaya sana,wakati huo ni uongo mtupu!

Na endapo wabunifu hao wangeamua kumsusia na kumuacha afanye vile alivyofikiri kufanya,ambavyo si sahihi kabisa,baadaye mambo yangeharibika, "indispensable" huyu angesema,"unaona, jamaa zangu hawa ovyo kabisa,wameharibu kazi", wakati aliyeharibu ni yeye.

Sifa nyingine kubwa za mtu anayejinadi kwamba ni "indispensable" ni kutafsiri kama kupingwa na kudharauliwa kila ushauri unaopingana na mawazo yake potofu anaopewa wa kuweka sawa mambo! Na mara zote watu hao hawawapendi wale wenye vipaji vilivyowazidi kuhusu shughuli inayohusika kama uwezo wa kiakili,uwezo wa kiushawishi,uwezo wa kifedha na kadhalika.Kwa hiyo,wakiwa kwenye ofisi moja, "indispensable" huyo huwachukia,kuwapakazia mabaya na kuwatenga watu hao huku akiwakumbatia wale wanaomkubalia chochote bila kuhoji uhalali au umantiki wa kitu hicho! Mara zote huwaelezea vizuri sana kwa watu kwamba hao ndiyo wanafaa kiutendaji! Kwa maelezo rahisi,huwachukia wenye akili nyingi na kuwapenda wajingawajinga wanaoramba viatu vyake!

Kwa ufupi,kama tunataka mambo yetu yaende kwa jinsi dunia ya sasa ya Sayansi na Teknolojia inavyoelekeza,lazima tuondoe huo ugonjwa wa kuamini kuwa kuna mtu "indispensable" mahali popote awe kijana au mzee,mwanamke au mwanaume.Katika dunia ya Sayansi na Teknolojia,kila kitu huendeshwa kisayansi.Iwe Sayansi per se,iwe Sayansi ya Jamii au Sayansi ya maendeleo yenye kanuni zake alizoziasisi Mwanafalsafa Karl Marx.

Shughuli yoyote inayoendeshwa kitimu kama timu ya soka,ya Basketball,ya Netball na vikundi vya sanaa pamoja na kazi za ofisini haina mtu aliye "indispensable".Huyu atoke na ashukuriwe kwa mchango wake wa mafanikio,huyu aingie kwa kuleta mbinu mpya na juhudi mpya.Kuna siku naye lazima aondoke kwani kanuni moja kati ya tatu za maendeleo ya kisayansi ya Karl Marx inasema lazima kuwepo kwa Upinzani ndani ya upinzani (negation of the negation).

Kanuni yake ya kwanza ya maendeleo ni kuwepo kwa muungano wa mitazamo tofauti ndani ya jamii husika na kisha muungano huo kuzua mgongano wa mawazo (Unity and Conflict of the opposites).Baada ya hapo ndipo inakuja hiyo kanuni ya pili ya upinzani ndani ya upinzani inayosababisha kuwepo kwa mabadiliko makubwa toka yale ya kimuundo hadi kufikia yale ya kubadilika kabisa kwa chombo husika (Transformation from quantitative changes into qualitative change).

Kwa hiyo,Yanga inapaswa iwe na watu wengi makini wanaopinga kimantiki na kivitendo hali ya klabu yao kubwa na tajiri sana kuendeshwa kadri tajiri mmoja anavyotaka iendeshwe kwa sababu ni yeye tu anayetoa pesa kwa shughuli zote za timu.Lazima uwepo muungano wa watu wenye mitazamo tofauti ndani ya klabu hiyo baina ya wale wanaoamini kuwa kuna "indispensable" kwenye klabu hiyo na wale wanaopinga kuwepo kwa "indispensable" ndani ya klabu yao yenye utajiri mkubwa mno wa mashabiki.

Muungano huo,utazua mgongano utakaosababisha mwisho kabisa klabu hiyo ikabadilika toka mabadiliko ya hapa na pale ya kimuundo hadi kubadilika kabisa kwa umbo lake na sura yake toka kuwa klabu ya "indispensable" mmoja hadi kuwa klabu tajiri inayojiendesha kama taasisi badala ya kumtegemea "indispensable" huyo mmoja.

Timu yoyote ni timu na kila mtu ana mchango wake katika kuipatia mafanikio timu hiyo,iwe ya michezo,ya sanaa,ya taasisi ya umma,ya taasisi binafsi na kadhalika.Ni makosa sana mtu kujinadi au kunadiwa ndani yake kwamba yeye ni "indispensable".Hakuna mtu "indispensable" katika taasisi yoyote.Simba ilikuwa na makipa kama Athumani Mambosasa,Omar Mahadhi,Moses Mkandawire,Mackenzie Ramadhani,Iddi Pazi mpaka Mohammed Mwameja miongoni mwa wengi sana.Nani alikuwa "indispensable" miongoni mwao? Leo hawapo na baadhi wametangulia mbele ya haki, mbona Simba ina uimara ule ule?

Yanga ilikuwa na kina Shariff Shiraz,Mohammed Virani,Abbas Gulamali,Muhsin Hassanali,Vinod Asar na wengine walioibeba sana kifedha kwa nyakati tofauti.Kama miongoni mwao kungekuwa na "indispensable", leo Yanga isingekuwepo.Mbona ipo imara tu? King Michael Enock wa Sikinde na Joseph Lusungu wa Msondo wameshatangulia mbele ya haki.Enzi ya uhai wao wakitumikia bendi hizo, walikuwa zaidi ya waalimu wa muziki.Leo hawapo na hatunao duniani, mbona bendi hizo bado zinadunda? Wangekuwa "indispensable" leo bendi hizo zingekuwepo?

Nawaomba sana Watanzania wenzangu,hasa wale wababaishaji na wasio na lolote la maana kichwani, waache kujinadi kwamba bila wao mambo hayaendi wakati nchi hii ilikuwa na Waziri Mkuu wa utendaji usio wa kawaida,Edward Moringe Sokoine.Amefariki dunia miaka 26 iliyopita lakini Tanzania ipo tu.Tulikuwa na baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ambaye kuwepo kwake kulikuwa ni nguzo ya umoja wetu.Ametutoka miaka zaidi ya 10 iliyopita na umoja wetu uko vilevile.Kama Nyerere na Sokoine hawakuwa "indispensable",wewe mtu wa kawaida kama mimi utakuwaje "indispensable"?

Kwa ufupi ushirikiano wetu wa dhati,kupeana uhuru wa kila mmoja kutoa mawazo yake ya kujenga na kuyaheshimu mawazo hayo huku yale yaliyo bora kuyachukua kwa utekelezaji na kukubali kusahihishwa unapokosea huku ukizingatia umuhimu wa kupokea mawazo mapya ya kimaendeleo ni muungano wa mambo ambao wenyewe tu ndiyo unaweza kuwa "indispensable" kwa mafanikio yetu na wala siyo kuwepo kwa mtu fulani miongoni mwetu.

Mtu anaweza akaondoka na maendeleo yakapatikana zaidi ya wakati alipokuwepo kwani yeye,na hali yake ya kujiona "indispensable", anaweza kuwa ndiyo kikwazo kikubwa cha mafanikio. Wenye uwezo thabiti wa utendaji na wenye akili nzuri,siku zote, huamini kuwa mafanikio hupatikana kwa ushirikiano wa pamoja wa kila mtu ndani ya timu.Watu hawa hawapendi kabisa kuambiwa wao ni "indispensable" na hawataki kuwemo ndani yao mtu anayejinadi au kunadiwa kuwa ni "indispensable".

Ni ukweli usiopingika kwamba hakuna mtu wa muhimu kuliko wote mahali popote pale bali umuhimu huo unaonadiwa na baadhi yetu ni wa kufikirika tu na unaweza kuwa kinyume cha ukweli wa mambo.

Saturday 24 April 2010

HILI NDILO JANDO LA KIENYEJI-1

Na Ibrahim Mkamba

1.0: Utangulizi

HAKUNA ubishi kwamba kwa dunia tuliyomo sasa,ni kashfa,ni kosa kubwa,ni ushenzi na ujinga kwa mwanaume wa kizazi hiki wa madhehebu yoyote na wa kabila lolote kutotahiriwa,yaani,kuwa na govi au kwa lahaja fulani kuwa na mkono wa sweta.Kama ni mila,ni mila gani ya kishenzi namna hiyo inayopaswa kuthaminiwa mpaka dunia hii? Kama ni madhehebu,ni madhehebu gani yanayosema kutahiri ni dhambi wakati manabii wote wa Mwenyezi Mungu walitahiriwa tena wakiwa na umri mdogo? Kwa msingi huo,kama ni dhambi basi mwanaume kutokutahiri ndiyo dhambi.

Kwa ufupi ni kwamba mwanaume kutotahiriwa,kwa sasa,ni jambo lisilokubalika kabisa na kwa hiyo ni vizuri tusaidiane kuhamasishana wanaume wote wa Tanzania tutahiriwe.Nakumbuka nilipokuwa Mzumbe Sekondari,tulikuwa tunalala kwenye nyumba moja,Karume namba sita,na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro wa sasa,Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Thobias Andengenye,tuliyekuwa naye kidato kimoja cha tano tukisoma masomo ya Historia,Jiografia na Lugha ya Kiingereza (HGL).

Andengenye alianzisha kampeni nzuri ambayo naikumbuka mpaka sasa ya kila siku usiku baada ya Maandalizi ya Jioni (Evening Preparation) kuwashambulia wote waliokuwa hawajatahiriwa ndani ya nyumba yetu hiyo ya Karume namba sita.Tuliungana naye kuwasema sana wenzetu hao bila mlengwa maalum.Cha kufurahisha,tulimaliza kidato cha sita bila kuwemo govi hata moja ndani ya nyumba yetu kutokana na kampeni nzuri ya mwenzetu Andengenye tuliyoshiriki kuiongezea nguvu.

Hivi tujiulize,unakuwaje tajiri sana,maarufu sana kiuongozi,kimichezo au kimuziki na sanaa nyingine kama kucheza filamu huku ukiwa hukutahiriwa? Umaarufu wako una umuhimu gani na govi lako? Kwa sasa,bila kujali mila za baadhi ya makabila yao dhidi ya tohara ya wanaume, hata watoto warembo,kama huyu ambaye sura yake inaonyeshwa upande wa kushoto na umbo lake lote upande wa kulia akitupambia makala hii, hawafurahi kuwa na washikaji wasiotahiriwa na wenye ushujaa na mapenzi ya kweli huwakera washkaji wao wasiotahiriwa warekebishe dosari hiyo.

Makala hii inahusu mila na desturi ya jando miongoni mwa wapogoro,wambunga,wandamba na wangindo wa Wilaya za Kilombero na Ulanga.Nimeona nieleze ninayoyakumbuka kuhusu mila hiyo ili kuwafahamisha wengine na kuitunza kwenye maandishi ikizingatiwa kwamba sasa hivi watoto wetu tunawapeleka kutahiriwa hospitali na miongoni mwa makabila mengi hakuna wanaotahiriwa porini kwa kisu bila ganzi na kuishi huko hadi wapone.Kwa hiyo,taratibu,mila hiyo inatoweka.Naomba tuwe pamoja kufichuliana siri za jandoni,ambalo enzi hizo,lilikuwa kosa kubwa mno.

2.0: Siku ya kutahiriwa

Takriban miaka 40 iliyopita,baba yangu mzazi ambaye kwa sasa ni marehemu,alituita mimi na ndugu zangu na kuomba maoni yetu ya endapo tulipenda tutahiriwe hospitali au kienyeji.Kwa kauli moja tuliamua twende porini kwa kuzingatia jinsi wale walioenda hospitalini walivyokuwa wanachopewa shuleni kwamba wameingia jando hafifu la kukatwa kwa ganzi.

Licha ya baba kupingana nasi akizingatia shuruba alizozikabili mwenyewe kwenye jando hilo la porini na licha ya ukisasa wake uliotokana na usomi wake akiwa Mwalimu wa Shule ya Msingi,sisi hatukubadili msimamo na tulisisitiza kwenda porini.Kwa bahati mama mzazi ambaye naye kwa sasa ni marehemu,alikuwa upande wetu.Baba akashindwa na kuruhusu tufanye kile tulichochagua.Kwa kuzingatia kuwa sisi ni Wapogoro wa Wilaya ya Ulanga,tulipenda twende kwenye jando la mila ya kabila letu ingawa wilayani Kilosa,tulikokuwa tukiishi,majando ya kienyeji ya kabila la Wasagara yalikuwepo.

Shule ya msingi Ulaya,iliyopo kilometa 32 (maili 20) kusini ya mji wa Kilosa ndani ya Wilaya ya Kilosa,Mkoani Morogoro tuliyokuwa tukisoma ambayo baba wetu alikuwa mmoja wa walimu, ikafungwa kama shule nyingine.Tukapanda basi la MORETCO la njia ya Kilosa-Malinyi tukiwa na mama mpaka Ifakara.Safari yetu ikaendelea mpaka kuvuka mto Kilombero kwa pantoni.Huko ng'ambo,ndani ya Wilaya ya Ulanga, tukavuka vijiji vya Kivukoni,Dokoyaya,Mngulungulu hadi Minepa.Hapo ndipo pakawa mwisho wa safari yetu.

Bila kupoteza muda,kila kitu kikawa kimeandaliwa.Alfajiri ya siku iliyofuata,pembe la mnyama lilipulizwa kama tarumbeta kuashiria kwamba shughuli ilikuwa imeiva. Tukaamshwa na kupata uji mzito wa mchele kabla ya kuanza kunyolewa nywele.Mara wengine wakajiunga nasi nao wakaanza kunyolewa nywele.Tukawa jumla ya watoto kama kumi hivi.Kilichofuata,kila mmoja wetu alibebwa begani kuelekea eneo la shughuli yenyewe tukiwa tumefungwa lubega ya kanga kila mmoja wetu bila nguo yoyote zaidi.

Mara nikaona kaka yangu,ambaye kwa sasa ni marehemu, anakimbizwa mbio kuelekea uelekeo fulani baada tu ya filimbi kama hizi za polisi kupulizwa.Mara nikasikia sauti nyingi na kubwa zikiimba: kuulisewa nami ntakwenda kulisewa,kulisewa nami ntakwenda kulisewa... Kila walipoweka pozi ya kuimba ili waanze tena kuimba maneno hayo,nilisikia sauti ya kaka yangu akilia kwa uchungu. Dakika kama tatu au nne baadaye,nikasikia filimbi na mara moja ikawa zamu yangu kukimbizwa kwenda eneo la kutahiria.

Nilipofika hapo,nilikuta kundi kubwa la watu,wengi wakiwa watoto, na mimi nilipelekwa moja kwa moja mpaka kati kati ya kundi hilo.Kanga ikavuliwa kwa nguvu na nikawa uchi kama siku niliyozaliwa.Nilikamatwa na mzee mmoja wa makamo ya kati mwenye nguvu nyingi aliyeibana kwa nguvu miguu na mikono yangu.Nilifanyiwa operesheni kwa kisu ambapo ndani ya dakika kama tatu za uchungu mwingi ,hasa eneo la chini,kila kitu kikawa tayari na niliondolewa kwenda kukalishwa jirani na kaka yangu.Hakuna aliyempa mwenzake pole wala hongera!

Mara moja tukapewa singa zilizotengenezwa kwa vitambaa vya kanga zilizochanwa chanwa kwa ajili ya kujifukuzia nzi.Si zaidi ya nusu saa baadaye,wote tukawa tayari tumekalishwa kwa mstari na vipepeo vyetu vya nzi.Hatua iliyofuata,iliumiza kuliko hata kisu chenyewe! Tuliwekewa pamba zenye spiriti kuzunguka majeraha yote.Uchungu wake ulizidi wa kisu chenyewe!

Baadaye wakaletwa watoto wa marika yetu kutuonyesha sehemu zao za uume na wazee kutuambia kuwa tusiwe na wasiwasi kwani nasi tutakuwa kama wao tukipona. Banda letu likijengwa na likiwa halijakamilika,siku ya kwanza tuliimaliza tukiwa chini ya mikorosho,miguu tukiitanua saa zote.Chakula siku hiyo,tangu wali wa mchana mpaka wali wa jioni hakikulika vizuri na sisi wali wa jando.

3.0: Maisha ya jandoni>
Siku za mwanzo jandoni zinaumiza sana,jeraha la tohara linauma,haja ndogo inatoka kwa maumivu makali na lazima uende kwa tahadhari kubwa ili sehemu hata ndogo ya haja hiyo isiende kwenye jeraha,kulala kwa kufungwa miguu ili uume usiguse sehemu nyingine ya mwili na mengi ya kutesa.Licha ya hali hiyo,ratiba ya siku ilianza kufuatwa mara moja huku msamiati wa jandoni ukisisitizwa mara moja kwa kutumika kwa mazungumzo yote badala ya msamiati wa kawaida.

(a)Ratiba ya siku

(i)Usiku wa saa tisa

Ratiba ya siku sijui ilianzia wapi kwani shughuli zake zilikaribia kuchukua saa 24 zote! Labda nianze pale wali wa jando walipoamshwa kwenye saa tisa usiku.Umepata kausingizi kadogo mara unasikia kama unaota Nyakanga au Mlombu (Kungwi) yeyote yule akiwaamsha kwa kuita "Ohoo" nanyi, miongoni mwa wale ambao walishatoka usingizini, wakiitikia,mara nyingi kwa unyonge sana "Ohoo".Majibizano hayo yalifanywa mara kadhaa kisha huyo Nyakanga au Mlombu alianzisha wimbo wa kuamsha: "Kamwali amka", nanyi mkiwa wote macho sasa mnaitikia, "tuimbe msimu",kisha anaendelea kuimba kwa kusisitiza "amka,amka", nanyi mnaitikia, "tuimbe msimu" kila anavyowaimbisha.

Kinachofuata ni mfululizo wa nyimbo za jandoni zenye mafundisho tupu ambazo mara nyingi zilikuwa zinaunganishwa kama DJ anavyounganisha muziki bila kusimama (nonstop).Kama akiamua kubadaili wimbo,kiashiria chake ni "ohoo!" na wali wa jando kuitikia "ohoo" mara kama mbili hivi katika utaratibu ambao kule JKT hufanywa kwa "Wii!" na kuitikiwa "Waa!".Utaratibu huo wa jandoni hutumika kila shughuli rasmi ya kuimba inapoanzishwa.

Basi usiku huo hapo jandoni mlianza kuimbishwa mfululizo toka "kwelekweche katumbo kana ngwali" mara "Yule kapita pale" mara "ukaya twaweli wanhtu" mara "kulisewa nami ntakwenda" na nyimbo nyingi sana kama hizo ambazo tune yake ilikuwa moja.

Aidha,ziliimbishwa nyimbo zenye mafunzo tupu pia kama "baba kajenga banda karibu na bustani,waarabu toka Unguja banda walitamani",,"madege yale juu ya mkwanga,mkwanga uteluke madege yatue", na nyingi sana zenye tune za aina fulani moja.

(ii) Alfajiri

Kwenye majira ya saa kumi na robo alfajiri,shughuli ya kuimba hufikia tamati na wali wa jando hutolewa nje kwenye baridi kali ya mwezi huo wa Juni kwenda kupiga magoti na kubinua makalio uchi kabisa ili majeraha yapulizwe na ubaridi mkali ikiwa ni tiba mojawapo.Mnakuwa mmebong'oka hivyo,ambapo kwa kipogoro huitwa kufulama huku mkiimba,"tufulame mhmbepu na mtera tufulame" kwa kipogoro ikimaanishwa "tubong'oke baridi na dawa tubong'oke".

Huko "kufulama" huchukua kama nusu saa hivi hadi saa kumi na moja kasorobo mnapoinuka,mnapovaa lubega na kuanza kuliita jua lichomoze mkipiga makofi na kutoa ishara ya kuita upande ambao jua litachomozea huku mkiimba "kajua kwela mmiyombo kwela kwela,kwela mmiyombo kwela kwela". Shughuli hiyo hudumu mpaka jua litakapochomoza saa kumi na mbili na dakika au kasoro dakika chache asubuhi. Na hukamilika mara linapomalizika kutokeza lote.

Kinachofuata kwenye ratiba ya siku ni kupakwa mwilini unga wa mchele uliolowekwa huku mkiimba "kapemba kalawili mashamba twawose tweneli kupakala" wimbo wenye maana ya kuwa unga huo umetoka shambani na wote tuenee kupakaa.Baada ya hapo,chai nzito na uji wa nguvu hufika toka nyumbani kwa wali wa jando mbalimbali na kifungua kinywa hicho hufikishwa bila mbwembwe za kijando jando tofauti na ilivyo kwa chakula cha mchana.

(iii) Asubuhi

Baada ya kupata kifungua kinywa,kama kulikuwa hakuna shughuli yoyote ya dharura kama kuadhibiwa kwa kosa la mmoja,baadhi au wote kwa kosa moja au makosa tofauti,saa za asubuhi zilitumika kufundishwa nyimbo ambapo baada ya muda,"maktaba" ya wali wa jando ilikuwa na nyimbo nyingi mno zilizogawanyika miongoni mwa za kuimbwa popote pale na mbele ya mtu yoyote yule hata nje ya kambi ya jando pamoja na zile zenye maana nzito mno ambazo ilikuwa marufuku kuimbwa nje ya kambi ya jando hata kama ujumbe wake ulikuwa wa mafumbo makubwa yasiyoeleweka.

Nyimbo zenye ujumbe mzito ziligawanyika kati ya hizo za maneno yaliyoficha ujumbe na zile ambazo kila kitu kilitamkwa wazi wazi wazi.Ninapozikumbuka nyimbo hizi za aina ya pili, mpaka leo,ikikaribia miaka 40 tangu niwe porini,mwili wangi unasisimka!

Kwenye majira ya saa tano asubuhi,wali wa jando walianza kuimba wimbo wa kuombea chakula ambao uliimbwa kwa sauti ya juu mno "nikolele mnaze nikamlindi mama,mama njalo katumbo kalegea" na kisha kuendelea na kibwagizo tu cha "mama njalo katumbo kalegea,mama njalo katumbo kalegea".Ujumbe mkuu wa wimbo huu ni kuwajulisha kina mama zetu kwamba njaa ilikuwa inauma na matumbo yalikuwa yamelegea kwa njaa.

Neno "njala", kama ilivyo kwa makabila mengi ya kibantu,lina maana kwa kipogoro "njaa". Wanapoimba "njalo" ni kama wanaweka msisitizo wa kusema "njala o" lakini herufi "a" ya mwisho inaondoka kwenye kutamkwa na kubaki "o" moja kwa moja na hivyo kuwa "njalo".

Wimbo huo ulisitishwa kidogo pale sahani ya wali kutoka kwa mama wa kwanza ilipofika jandoni.Hapo sahani hiyo ilikwenda kupokelewa kwa mletaji kuimba toka huko alikoipokea nje ya eneo la jandoni:- "kiranja mhmbokelage digali dya mbulaga,fumbi mhbokelage digali dyambulaga" na wali wa jando waliitikia "dedede mtwa weto dedede,dedede mtwa weto digali dyambulaga". Vinginevyo,iliitikiwa "dedede mtwa weto dedede mtwa weto,dedede mtwa weto dedede mtwa weto,oo mtwa weto,oo mtwa weto"

Mletaji akishaifikisha sahani hiyo,hujitikisa na kuimba akiuliza,"pakutula nhntuleje" na wali humuitikia "gutuli utetema". Hapo aliuliza kwa kuweka (sahani hiyo) awekeje na wali wa jando kumuitikia aweke ukitetemeka na hapo sahani hiyo ya wali inakuwa imeshapokelewa.Baada ya kuipokea sahani hiyo,wimbo wa kuomba chakula uliendelea na utaratibu ukawa huo huo kwa kila sahani iliyopokelewa mpaka zote kuenea.

(iv) Mchana

Baada ya sahani zote kuenea kwenye majira kama ya saa saba hivi adhuhuri,kiongozi wa Makungwi (Walombu),huanza taratibu za kugawa chakula hicho kwa kuanza kujichotea chake akiimbisha:"natomo natomo njoo unitomolee" na wali wa jando kuitika "natomo natomo njoo ututomolee" na wimbo huo kurudiwa mara kadhaa huku akichota kwa mkono chakula kutoka kila sahani.

Ghafla anaweza "kuwauza" kwa kuimba: "chakula kibaya kapika mama fulani" (akitaja jina la mwali mmoja wa jando). Hapo mwali yoyote asijisahau na kuanza kuitikia "chakula kiba...".Wote mtapata karinye karinye kubwa mno kabla ya kula chakula.Mnachopaswa kujibu ni "mbukwa" basi."Mbukwa" ni neno la jandoni la kutokubali jambo kwa maana ya si la kiadilifu na la kuombea msamaha ama kwa kutamkwa tu au kwa kuimba "mbukwa mbukwa (Mlombu au Nyakanga) wetu mbukwa"

Kinachofuatia ni kula chakula ambapo kikikaribia kwisha,wa mwisho kutahiriwa,aliyeitwa Sungura,alipaswa kuachiwa chakula kidogo kwani yeye alichukuliwa kuwa mdogo na hivyo alikuwa ndiye mtoa vyombo.Baada ya kupona pona kidogo,msipomuachia,hubeba sahani wakati wowote na kukimbia nayo akamalizie kula huko kwingine.Mara nyingi alifukuzwa sana kunyang'anywa sahani hiyo ya chakula.Kuepuka hali hiyo hatarishi kwa wali wa jando,ilikuwa busara kumuachia kwa amani chakula kidogo kwenye sahani.

(v) Alasiri

Baada ya chakula cha mchana kwenye saa nane alasiri kunakuwepo na mapumziko yasiyo rasmi ya saa kama tatu hivi yaliyojumuisha kufundishwa nyimbo na kuelezwa maana zake pamoja na kufundishwa jinsi ya kufanya katika shughuli ya kutembelea nyumbani kwa wali wa jando usiku wa siku kadhaa zinazofuata.

(vi)Jioni

Saa 11 na dakika chache jioni, wali wa jando walianza kuimba wimbo wa kuliaga jua linalozama kwenye saa 12.30 jioni au karibu ya muda huo.Kulikuwa na nyimbo mbili maarufu.Wa kwanza: "sualele sualele kajua kagenda sualele".Maneno hayo yalianzishwa na mwimbishaji na wali wa jando kuitikia,"sualele sualele kajua kagenda sualele".Baadaye mwimbishaji aliendeleza tu kuimbisha hivi na kuweka madoido kadhaa: "Oo kajua kagenda" na wali wa jando wakiitikia hivi kwa muda karibu wote kama mwimbishaji hataanzisha tena ubeti wa kwanza:"sualele kajua kagenda sualele" huku mwimbishaji aki-'rap' kwa maneno "kajua kagenda" na "kagendaaa kajua kagenda"

Wimbo wa pili ambao haukuchangamka sana na ulichosha kuimbwa kwa muda mrefu hivyo uliimbwa ukianzishwa na mwimbishaji; "Sualele wali wangu sualele" na wali wa jando waliitikia;"kajua kagenda" kisha mwimbishaji kuimba; "Fumbi na Kiranja wali wangu sualele" na wali wa jando kuitikia vilevile kisha mwimbishaji huimba; "sualele"na wali wa jando kuitikia "aa aa sualele kajua kagenda"Wimbo uliendelea hivyo hadi jua lilipozama huku katika nyimbo zote hizo,wali wa jando walipiga makofi mara moja moja na kuonyesha ishara ya kulisukuma jua liende au lizame kinyume na ishara ya asubuhi ya kuliita jua lije juu au lichomoze.

Kwenye ratiba ya siku,shughuli hiyo ilifuatiwa nakupakwa unga wa mchele katika utaratibu ule ule wa asubuhi na kwa wimbo ule ule.Kwenye saa moja mpaka saa mbili usiku ni muda wa chakula cha jioni.

(vii) Usiku

Baada ya hapo ni kukaa sehemu za kulala kwa kujilaza na kuimbishwa nyimbo nyingi mpaka kwenye saa 7 usiku ulipoimbwa wimbo wa kuwalaza ulioimbwa "njechembe, njechembe mbati gogo we njegame"na wali kuitikia kwa kuimba maneno hayo hayo kisha kibwagizo kikawa cha maneno hayo hayo.

Saa mbili tu baadaye,mnaamshwa tena kuanza siku mpya na ndiyo maana awali nilisema ilikuwa vigumu kujua ratiba ya siku ilianzia wapi.Kwa kumaliza sehemu hii ya kwanza ya makala hii,naomba nifafanue vitu ambavyo vitaelezwa kwa kina kwenye sehemu inayofuata.Humu ametajwa Kiranja, Fumbi na Fumbi gogo.Hawa ni wa kwanza kutahiriwa (Kiranja),wa pili (Fumbi) na wa tatu (Fumbi gogo).Wengine hawakuwa na majina mpaka wa mwisho aliyeitwa Sungura.

Hili ndilo jando la kienyeji.Naomba tukutane kwenye sehemu ya pili kwa kupeana siri zaidi za jando hilo.

Thursday 22 April 2010

HONGERA SIMBA SPORTS CLUB 2009/2010 !


Na Ibrahim Mkamba

BAADA ya kuukosa ubingwa wa Tanzania Bara kwa misimu miwili,yaani 2007/2008 na 2008/2009,Simba Sports Club wamebeba ubingwa huo msimu huu wa 2009/2010 toka mikononi mwa watani wao wa jadi,Yanga,walioushikilia ubingwa huo kwa miaka miwili mfululizo katika misimu iliyotajwa hapo juu.Simba wanastahili pongezi kubwa kwa kubeba ubingwa huo bila ya kupoteza hata mchezo mmoja hadi siku walipofikisha pointi zisizoweza kufikiwa na timu nyingine na hadi walipomaliza kabisa ligi.

Wamecheza mechi 22,wameshinda 20 na kutoka sare mbili dhidi ya Kagera Sugar na African Lyon.Kwa matokeo hayo,kati ya pointi 66 zote,Simba wamepoteza nne tu kwa timu walizotoka nazo sare na hivyo kukusanya jumla ya pointi 62.Walifanya kazi kubwa sana wana Msimbazi hao hasa baada ya kupata sare ya kwanza ugenini Bukoba, nyumbani kwa Kagera Sugar.

Sare hiyo ya 1-1 ilikaribisha vichwani mwa baadhi yetu picha kwamba kuanzia hapo bingwa hakuwa akijulikana baina ya Yanga na Simba na baadhi yetu tukaandika hivyo magazetini! Tena makala au habari zilizokuwa na mwelekeo huo zilikuwa na uzito mkubwa kuliko zile zilizoeleza kwamba kuwashusha chini Simba waliokuwa juu kwa tofauti ya pointi 10 ilikuwa kazi ngumu mno.

Mambo yakawaendea vibaya zaidi wana Msimbazi baada ya sare nyingine ya 1-1 dhidi ya African Lyon.Hapo,tofauti ya pointi nane juu ikawafanya waonekane kupoteza kabisa uwezekano wa kuubeba ubingwa huo, wakati wataalam wa kweli wa soka waliona, walisema na tulisoma wakieleza kwamba timu yenye mwendo wa kutoshindwa tangu mwanzo wa ligi,ni ngumu kukosa pointi mbili ndani ya mechi tatu isipokuwa kwa maajabu ya soka tu.

Kilichosisimua ni kwamba ilifika wakati mawazo ya baadhi yetu yalijilazimisha kuamini na kuwaaminisha wengine kwamba Yanga walikuwa na uwezo wa asilimia zote wa kushinda mechi zote zilizokuwa zimebaki lakini Simba, ambao tangu ligi inaanza mwezi Agosti mwaka jana walikuwa hawajapoteza mechi huku wakishinda nyingi, ndiyo walionekana kuwa na uwezekano wa kufungwa kwenye mechi hizo zilizobaki!

Kama mpenda soka,niliona ni vizuri msimu huu kwa timu nyingine kuchukua ubingwa na si Yanga kwani ingefanya hivyo, ungekuwa msimu wa tatu mfululizo.Kwa nini timu moja itawale namna hiyo mpaka ijisahau? Ningeiombea Yanga ibebe tena ubingwa huo ingawa ni kwa msimu wa tatu mfululizo kama wangeenda na kasi ya Simba tangu mwanzo wa ligi huku timu nyingine zikisuasua.Ningefanya hivyo kwa hoja kwamba aliyestahili ubingwa,aupate tu na hivyo ndivyo Simba walivyostahili kuupata msimu huu kwa kasi waliyoitumia.

Ni wazi kiushabiki,kila shabiki wa timu huiombea mema timu anayoshabikia na huwaombea mabaya mahasimu lakini maombi hayo huwa magumu kutekelezwa kama unayemshabikia alianza kwa kasi ndogo mno huku hasimu akianza kwa kasi kubwa ya kutafuta mafanikio. Hata zile ngonjera za kuomba Simba ibanwe na kushindwa kutangaza ubingwa mpaka wakati wa mechi ya Watani wa Jadi zilitolewa kishabiki kwa kisingizio cha kuongezeka kwa utamu wa mechi hiyo ya watani.

Ngonjera hizo hazikuwa na mantiki yoyote bali zilikuwa za kuomba mabaya tu kwa mahasimu kwani,kwa hoja za kuifanya mechi ya Watani kuwa tamu,ombi hilo lilikuwa kinyume cha mambo.Kama Simba ingekuwa imebakiza pointi moja, mbili au tatu kubeba ubingwa kufikia pambano hilo,ni wazi pambano hilo lisingekuwa na ufundi wowote ule bali lingejaa butua butua zozote ili mradi ushindi upatikane, kukamiana kulikopitiliza,ushirikina wa hali ya juu,kutoaminiana kwa wachezaji kwa wachezaji na kutoaminiana baina ya timu hizo na waamuzi.

Matokeo yoyote ya ushindi kwa moja ya timu hizo,kama huo wa Simba wa 4-3, yangezusha tuhuma za kijinga kwa waamuzi,baadhi ya wachezaji kuadhibiwa na uongozi na hata migogoro mikubwa klabuni ingeanzia hapo.Lakini kwa sababu Simba waliingia kwenye pambano hilo wakiwa mabingwa tayari huku Yanga wakiwa wa pili tayari, mechi hiyo ya Aprili 18, 2010 ilistahili kuwa ya amani kikweli kwa kujaa ufundi mtupu kutokana na uzuri wa makocha wa timu hizo na ubora wa wachezaji wake ingawa hali haikuwa hivyo!

Sasa jiulize kama mechi isiyo ya kumpata bingwa ilikuwa hivyo,huku Yanga wakiwatafuta wahujumu wa mechi hiyo,hali ingekuwaje kama mechi hiyo ingekuwa ya kumpata bingwa?

Binafsi nilifarijika Simba kumaliza ubishi siku walipocheza na Azam na kushinda kwa mabao 2-0 ya Mkenya Mike Barasa.Pamoja na sababu niliyoieleza ya utamu halisi wa mechi ya watani,matokeo hayo yalirudisha afya nzuri kwa mashabiki wa Simba na wa Yanga.Shinikizo la damu na roho kuwa juu viliwakabili sana mashabiki wa Simba muda wote kabla ya siku hiyo na afya za baadhi yao kuathirika huku wale wa Yanga nao wakiwa na tatizo hilo hilo wakisubiri kwa matazamio Simba kuteleza.

Nani kasema kuwa anayesubiri kwa hamu jambo jema ambalo alikuwa halitarajii sana hana shinikizo la damu na roho yake haiwi juu juu? Hujasikia mtu akiomba mgonjwa wake achukuliwe na Mwenyezi Mungu ili watu wapumzike baada ya kumuuguza sana bila matazamio ya mgonjwa huyo kupona? Hujasikia mtu akiomba hukumu itolewe ili ajue kama anafungwa au anaachiwa huru ili nafsi yake ikubali matokeo yoyote yale na iwe huru kutoka kwenye shinikizo kubwa la damu la kuishi kwa matumaini? Kwa hiyo ushindi wa Simba dhidi ya Azam ulitatua matatizo ya kiafya ya mashabiki wa timu zote mbili za Yanga na Simba ambao kuanzia hapo walikuwa katika hali ya kawaida baada ya hali ya kuwa roho juu juu kumalizika.Narudia tena kusema pongezi nyingi kwa Simba kutwaa ubingwa wa ligi kuu ya soka ya Tanzania Bara kwenye msimu huu.

Simba wamestahili msimu huu kupata mafanikio haya makubwa kutokana na kikosi hicho kutengenezwa vizuri kikijumuisha wachezaji wazuri wa idara zote waliosajiliwa kwa uwiano sahihi badala ya kurundikwa tu.Bahati waliyo nayo watu wa Simba ni kuwa na Kamati ya Usajili iliyo na mawasiliano mazuri na Mwalimu wa timu,Patrick Phiri,Kamati hiyo kujumuisha watu wanaoujua mpira,wenye uwezo wa kifedha na mapenzi ya dhati kwa klabu yao.

Pili,Simba ina kocha mzuri mwenye mahusiano mazuri na wachezaji ambao kutokana na mahusiano mazuri hayo,hawafurahi kabisa kumuangusha kwa kupata matokeo mabaya.Kocha huyo pia anapendwa na uongozi pamoja na Marafiki wa Klabu(Friends of Simba).Hivyo,ubora wa kazi yake ukichangiwa na hoja hizo nyingine,Simba imepata mafanikio haya.

Yanga wamechukua ushindi wa pili na kupata nafasi ya kutuwakilisha kwenye mashindano ya kombe la Shirikisho mwakani.Wakati msimu unaanza,Yanga walianza kwa maandalizi duni mno huku uongozi wa klabu ukiwa haujui kambi iwe wapi wakisubiri tajiri wao Yussuf Manji aseme naye kuwa kimya kwa muda mrefu huku wakati ukizidi kutaradadi kabla ya kipyanga cha kuanza ligi kuu msimu huu uliomalizika kupulizwa.

Baada ya kuwa kimya kwa muda mrefu,uongozi wa klabu ukatangaza kambi hiyo kuwa Mwanza.Wataenda leo,wataenda kesho,leo,kesho....siku zikawa zinazidi kwenda! Ghafla, tajiri akaibuka hewani na kuuliza,"Mwanza,kufanya nini,wakati jengo la klabu limekarabatiwa?".Angesema hivyo mapema basi,matokeo yake siku za maandalizi zikawa chache na ghafla Wanajangwani wanaingia uwanjani dhidi ya African Lyon.Wakalazimisha sare ya 1-1 kwenye pambano walilozidiwa kidogo!

Wakaenda Songea hivyo hivyo tu na kulala 1-0 kwa Majimaji.Wakafika tu Dar,bila kupumzika wakapata sare nyingine ya tia maji tia maji ya 2-2 kwa kuchomoa goli kwa tuta dhidi ya JKT Ruvu kwenye dakika ya mwisho kabisa.Kama Kiggi Makassy angevurunda jukumu zito la kupiga penalti ya dakika hizo ya kuweka mambo sawa,Mzee mzima angelala mechi ya pili mfululizo!

Baadaye,from nowhere akaibuka tajiri wao Manji na kufuturu na wachezaji tu bila viongozi kuwepo hapo Kempisky Kilimanjaro Hotel na kuwaahidi mambo mazuri wakienda kuifunga Mtibwa Sugar Morogoro na wachezaji hao kutimiza vizuri maelekezo hayo kwa kwenda kuipiga Mtibwa 1-2,Morogoro kwa magoli ya Amir Maftah na Mrisho Ngassa.

Kwa ufupi Yanga wangeweza kuwa chini kuliko pale walipokuwa kwenye msimamo wa ligi kama ligi hii ingekuwa na wapiganaji wengi wa nguvu kama ligi za zamani au kama Azam na African Lyon wangekuwa tayari wazoefu wa ligi kuu hiyo.Hii inatokana na ukweli kwamba timu hiyo kongwe kuliko zote nchini ilikosa mipango ya kisayansi ya maandalizi ya kimsimu kama ya wenzao Simba.

Wakati Simba walikuwa na kocha waliyekuwa na mahusiano naye mazuri,Yanga walikuwa na Dusan Kondic waliyekuwa na vita naye vya maneno vya hapa na pale kuhusu maslahi yake binafsi na mazingira ya kazi.Wakati Simba walifanya scouting ya wachezaji kama Emmanuel Okwi,Umuny,Joseph Owinogera na Stephen Bengo toka Uganda na Hillary Echessa toka Kenya,Yanga walikuwa wakimpokea mtu yeyote aliyedai mchezaji aliyejipeleka Jangwani na ndipo walipowapata kina Robert Jama Mba toka Cameroon, Kabongo Honore na wengine wa nje waliokosa matumizi kwa klabu.

Licha ya kufuatiliwa na kuhitajiwa na Simba,Bengo aliamua kwenda Yanga anayoishabikia kutokana na jinsi anavyomshabikia Edibily Lunyamila aliyekuwa na Yanga iliyobeba ubingwa wa Afrika Mashariki na ya kati mara mbili nchini Uganda (1993 na 1999),Bengo akiwa mdogo akishuhudia vitu vya Lunyamila.

Wakati Simba walipanga kuwa kambi zao zitakuwa Hoteli ya Lamada na Zanzibar kwa msimu wote na kuanza kambi hizo mara moja wakiwa na karibu wachezaji wote,Yanga walikuwa hawajui kama wangekuwa Mwanza au hapo hapo maskani kwao Jangwani,huku wachezaji wakianza kwa migomo ya mazoezi kwa kucheleweshewa mishahara kwa Watanzania na kugomea kuishi klabuni kwa wageni! Katika hali kama hiyo ilibidi ushindi wao wa kwanza kwenye ligi ulazimishwe kwa motisha,jambo ambalo binafsi naliona ni la hatari mno.Vipi wachezaji wakishinda mfululizo bila kupata chochote,si wanaweza kuanza mfululizo wa kupoteza mechi ili wabembelezwe kushinda tena kwa ahadi ya motisha fulani?

Kwa mipango yake,Yanga ishukuru sana kuwa na timu mbovu za ligi kuu, vinginevyo pengo la pointi 13 toka kwao hadi bingwa lingejazwa na Pamba,Coastal Union,Prisons,Sigara na Mtibwa enzi zile tulipokuwa na timu za kikweli za ligi kuu.Hata hao Simba, pointi zote kasoro nne wangezitoa wapi wakati huo? Yanga msimu ujao inapaswa ibadilike,pesa hainunui kila kitu kama hamtapanga mambo yenu sawa sawa kwa mipango ya muda mrefu,angalau ya msimu mzima wa ligi.

Azam wanastahili pongezi kubwa mno kwa kuchukua nafasi ya tatu kwenye msimu wake wa kwanza tu wa ligi kuu huku nafasi mbili za kwanza zikiwa za Yanga na Simba.Kwa jinsi timu hiyo ilivyo na mipango mizuri, ikiwa na timu ya uhakika sana ya watoto,naamini mwakani itafanya makubwa zaidi.Naitakia heri.

Mtibwa ya msimu huu ambayo ni ya nne si ile inayojulikana kwa soka yake inayoifunika Simba na Yanga.Mechi ya mwisho wamefungwa na Simba 0-4,Morogoro.Sikushangaa.Kwanza,Mtibwa hii iliyotoa pointi zote 12 kwa Yanga na Simba na kufungwa jumla ya magoli 12-3 na timu hizo,7-1 Simba na 5-2 Yanga,ilionekana wazi kutokuwa serious na ligi kuu ya msimu huu uliomalizika.Dalili zinaonyesha wakali hao wa Manungu,Turiani Morogoro wako njia moja kuwafuata Pamba,CDA,African Sports,Reli na wakali wengine wa enzi hizo kama wenzao Prisons walivyotangulia msimu huu kuifuata njia hiyo!Katika hali kama hii,kwa nini Watanzania wasishabikie timu mbili tu za Yanga na Simba kwani ndizo pekee zenye uhakika wa kudumu?

Pili,baada ya mechi za mwisho kusogezwa mbele,ni wazi timu pekee zilizokuwa zikijiandaa sana zilikuwa zile zilizokuwa zikihitaji kitu fulani,zaidi kubaki ligi kuu kwani wa kwanza na wa pili walishapatikana.Kwa hiyo,inavyoonekana,Mtibwa hawakujiandaa sana kwa mechi ya mwisho wakiona kuwa hawakuwa na mahitaji yoyote makubwa kwenye kumaliza ligi hiyo.Kwa bahati mbaya mechi yao ya mwisho ikawa na timu iliyojiandaa sana kupambana na Lengthens ya Zimbabwe,Yanga na Haras El-Hadood ya Misri,sasa ulitegemea nini hapo?

Kwa uzuri wa timu zao na uzoefu wao kwenye ligi kuu,JKT Ruvu iliyomaliza ya tano na Kagera Sugar ya saba hazikustahili nafasi ilizokuwemo.Hizi zilipaswa kuwa miongoni mwa timu za kugombea nafasi mbili za juu.Tatizo lao ni kuona wapinzani pekee wa kupigana nao kwa nguvu ni Yanga na Simba tu,jambo lililosababisha walioshuka daraja msimu huu wakumbwe na dhahama hiyo.Kwa kutafuta uzoefu kwenye msimu wa kwanza nafasi ya sita kwa African Lyon si mbaya hasa walipowatupa chini wazoefu kadhaa wa ligi kuu.Naamini mwakani watakuwa bora zaidi na wataingia mashindanoni kusaka ubingwa wa ligi kuu.

Mambo ya Majimaji yalikuwa hayaeleweki msimu huu.Fukuza fukuza yao ya kitoto kwa wachezaji bila ushahidi ndiyo imewaweka kwenye nafsi ya nane,mbili tu kufikia kushuka daraja.Unafungwa na Simba au Yanga,unasema wachezaji wamehujumu,hivi hizo Yanga na Simba unazionaje? Nani hakufungwa na Yanga na Simba msimu huu? Timu zote zimefungwa na miamba hao wa soka wanaoongeza ukali wao kwa uwakilishi wa kimataifa.Unafukuzaje wachezaji kwa kufungwa na miamba hiyo na usimlaumu yeyote kwa kufungwa nyumbani Songea na Toto Afrika,iliyofika huko saa chache kabla ya mechi na Moro United iliyokwishshuka daraja? Ugonjwa ni ule ule,watu wanaingia ligi kuu kwa kuzikamia Yanga na Simba tu.

Toto Afrika wameponea chupuchupu kushuka daraja.Kama Yanga wasingesawazisha bao dhidi ya Prisons kule Mbeya,wastani wake wa magoli ambao ungekuwa -9 ungewabakiza Prisons ligi kuu na Toto Afrika kushuka daraja kwa wastani wa -12 kwani zote zingekuwa na pointi 23.Tatizo la Toto wana akili ya ki-toto.Siku zote mawazo yao ni kusaidiana na Yanga.Hayo mawazo ni ya kizamani.Kitakachowapumbaza sasa ni Yanga kusawazisha bao dhidi ya Prisons na wao kubaki wakiamini kuwa hao Yanga ni "kaka" zao wa kweli waliomuua mtu kuwaokoa! Je Manyema Rangers wangeshinda Tanga dhidi ya Azam waliotoka nao suluhu,Yanga wangekuwa wamewasaidia nini? Je wenyewe Toto wangefungwa au kutoka sare na Kagera Sugar kwenye mechi ya mwisho,Yanga wangekuwa wamewasaidia nini?

Ninasema hivi nikizingatia mambo mawili.Kwanza,jinsi vijana hao wa Mwanza wanavyopigana kwa nguvu zote dhidi ya Simba,kama nguvu hizo wangekuwa wanazitumia kwa mechi zote, wala wasingetegemea msaada wa Kagera Sugar wa kucheza soka ya chini na kuwawezesha kushinda.Hapa simaanishi kwamba mechi hiyo ilipangwa bali ninamaanisha kwamba Kagera Sugar walicheza kwa ku-relax kwani hawakuwa na mahitaji yoyote ya ushindi wa mechi hiyo.

Pili,walipotoka Songea walikoishinda Majimaji 0-1,waliamini Yanga wangewahurumia kwa kuzingatia nafasi mbaya waliyokuwemo kwenye msimamo wa ligi.Walikuwa nyanya wakisubiri msaada wa "kaka" zao.Walipigwa 6-0 na kama wangeshuka daraja kwa kuzidiwa wastani wa magoli,basi "kaka" zao wangekuwa wamechangia sana kuwashusha!

Manyema Rangers,Prisons na Moro United wameshuka daraja.Kikubwa ni kwamba wasivunje timu,wakapambane na kurudi tena baada ya msimu mmoja kama Manyema Rangers walivyowahi kufanya,kukosa msimu wa 2008/2009 tu na kama Polisi Dodoma walivyofanya kukosa msimu huu tu.

Hii ndiyo ligi kuu ya 2009/2010 ambayo kwa kiasi kikubwa ilikuwa ya Simba kwa kupata pointi nyingi kuliko timu zote,kwa kuwa na mchezaji-Mussa Hassan Mgosi- aliyefunga magoli mengi kuliko yeyote wa timu nyingine(magoli 18),kwa kufunga magoli mengi kuliko timu zote nyingine na kwa kufungwa magoli machache kuliko timu zote nyingine.

WALIVYOMALIZA

P W D L GF GA Pts
1.SIMBA 22 20 2 0 50 12 62
2.yANGA 22 15 4 3 46 18 49
3.AZAM 22 8 9 5 30 23 33
4.MTIBWA 22 9 6 7 24 23 33
5.JKT 22 6 7 9 27 29 25
6 LYON 22 6 7 9 22 24 25
7.KAGERA 22 5 9 8 15 22 24
8.MAJIMAJI 22 6 6 10 14 26 24
9.TOTO 22 6 5 11 25 37 23
10.MANYEMA 22 6 5 11 20 36 23
11.PRISONS 22 5 6 11 19 29 21
12.MORO 22 4 6 12 19 32 18

Monday 19 April 2010

KARUME MWANZILISHI WA YANGA NA JINA LA SIMBA SPORTS CLUB

Na Ibrahim Mkamba

HISTORIA yetu katika mambo mengi imepotoshwa ama kwa makusudi au kwa bahati mbaya.Ni upotoshaji wa historia mtu anapoizungumzia klabu ya Young Africans maarufu kama Yanga bila kumzungumzia hayati Sheikh Abeid Aman Karume ambaye tangu atutoke kwa kupigwa risasi mwaka 1972, tarehe 7 mwezi huu na mwak huu ilitimia miaka 38 kamili.Ni upotoshaji wa historia mtu anapozungumzia jina la Simba Sports Club bila kumtaja Rais huyo wa kwanza wa Zanzibar na Makamu wa Kwanza, wa kwanza, wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Aidha,ni kosa kubwa kiimani na kimaadili mtu kuzipongeza klabu za Simba na Yanga kuwa na majengo yake bila kumhusisha kwa kiwango kikubwa hayati Karume.Kutomhusisha huko,kiimani ni dhambi ambapo kimaadili ni utovu mkubwa wa shukrani.Kwa maneno mengine,klabu za Yanga na Simba zilifanyiwa makubwa mno na hayati Karume kinyume cha jinsi historia inavyofanyiwa jitihada kwa Mwenyekiti huyo wa kwanza wa Baraza la Mapinduzi ya Zanzibar kutosikika sana ndani ya klabu hizo za soka zenye mashabiki wengi ndani ya Jamhuri nzima ya Muungano wa Tanzania.

Aliyoyafanya Karume kwa Yanga

Historia iliyoandikwa haielezi vizuri ukweli kwamba Sheikh Abeid Aman Karume alikuwa mhamasishaji mkubwa wa kuanzishwa kwa klabu ya soka ambayo sasa ndiyo hii inayoitwa Young Africans yaani Yanga.Baada ya kufanya kazi ya ubaharia iliyomuwezesha kuzunguka karibu dunia nzima kwa miaka kadhaa akiwa kijana mdogo, Karume alipata uzoefu wa yaliyotokea kwenye nchi mbalimbali alizozunguka duniani na kugundua kwamba serikali za kikoloni zilipiga vita uanzishwaji wa vyama vya siasa na wananchi wazawa lakini zilikuwa hazipingi vyama vya kijamii kama klabu za michezo.

Baada ya kuufahamu ukweli huo,akiwa nyumbani Zanzibar,Karume alijiunga na wenzake na kuunda klabu ya soka iliyojulikana kama African Sports Club,mwenyewe akiwa mchezaji mahiri wa timu ya klabu hiyo.Humo humo kwenye mikutano ya kisoka ndimo yeye na Wazanzibari wenzake walikuwa wakijadili jinsi ya kujinasua toka kwenye utawala wa kisultani uliokuwa ukilindwa na Waingereza.

Ni hayati Karume ndiye aliyehamasisha kuanzishwa kwa matawi ya hiyo African Sports ya Zanzibar na akafanikiwa kuanzishwa kwa tawi la timu hiyo jijini Dar es Salaam ambalo kwa sasa ndilo hii klabu kubwa sana ya Yanga na kule Tanga alifanikisha kuanzishwa kwa tawi jingine ambalo ni African Sports ya Tanga.Kumbuka kuwa kwenye miaka hiyo ya nyuma miji ya Dar es Salaam,Bagamoyo,Pangani na Tanga ilikuwa na ukaribu sana wa kimahusiano na miji ya visiwa vya Unguja na Pemba.

Baada ya kuanzishwa,timu hizo tatu za Yanga ya sasa,African Sports ya Zanzibar na African Sports ya Tanga zilitengeneza undugu wa damu mkubwa mno.Zote tatu zilikuwa chimbuko la hayati Karume ingawa historia haiuweki wazi ukweli huo.

Kwa Yanga pia, hayati Karume ndiye alitoa kiasi kikubwa cha pesa,kama siyo chote, mwaka 1971 kwa kufanikisha ujenzi wa jengo la makao makuu ya Yanga la sasa lililopo kwenye makutano ya mitaa ya Twiga na Jangwani,Kariakoo jijini Dar es Salaam.Alifanya hivyo kwa Yanga baada ya kushirikiana na wana Simba kupata jengo lao kwenye mtaa wa Msimbazi,Kariakoo,jijini Dar es Salaam mwaka huo 1971 kwa kuchangia kiasi cha pesa. Ki msingi,hayati Karume alishiriki kujenga majengo yote mawili ya klabu za Yanga na Simba ingawa historia iliyoandikwa haitaki kuuweka wazi ukweli huo.

Hivyo ndivyo hayati Karume alivyoifanyia klabu ya Yanga tangu kuanzishwa kwake mpaka kupata jengo la makao makuu yake.Ukitaka kuamini jinsi jengo la Yanga lilivyo na mahusiano na Wazanzibari,tangaza leo kupigwa kwake mnada,uone jinsi utakavyoshukiwa kwa hasira na Wazanzibari.Kama huamini,nitakukumbusha.Mwaka 1988 jengo hilo lilikuwa lipigwe mnada baada ya Yanga ya kina Ally Bwamkuu kudaiwa kiasi fulani kikubwa cha pesa.Kila kitu kilikamilika kwa hatua hiyo kutekelezwa lakini hilo halikufanyika baada ya jopo la Wazanzibari kadhaa kutia timu Dar es Salaam na kuweka pingamizi dhidi ya hatua hiyo kwa sababu kulikuwa na mkono wa Wazanzibari kwenye ujenzi wa jengo hilo.Mnada haukuwepo na deni lililipwa kwa njia nyingine.

Aliyoyafanya Karume kwa Simba


Kwa upande wa Simba iliyoanzishwa toka kwa watu waliojitenga toka klabu iliyoanzishwa kwa hamasa ya Karume iitwayo sasa Yanga,hayati Karume alifanya mambo makubwa pia.Siku ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa jengo la klabu hiyo la mtaa wa Msimbazi,Karume alitoa mchango wake wa fedha wa kufanikisha ujenzi wa jengo hilo. Hapo hapo alitoa rai kwa klabu hiyo kuachana na jina la Sunderland Sports Club lililokuwa likitumiwa na klabu hiyo hadi wakati huo.

Hakuishia kuelekeza tu kwamba jina hilo lilikuwa haliakisi utamaduni wetu na lilikuwa mwendelezo wa mabaki ya ukoloni bali pia alipendekeza jina linalotumika sasa na klabu hiyo nami nakumbuka wazi wazi nilivyomsikia akisema kupitia Radio Tanzania Dar es Salaam.Nakumbuka kumsikia akisema "Achaneni na jina hilo la kikoloni la Sunderland,kwani tuko Uingereza hapa? Mnaweza mkajiita Simba Mwekundu Sports Club,jina linaloeleweka na linaloendeana na utamaduni wetu..." Alipendekeza jina la Simba Mwekundu kufuatia rangi kuu ya klabu hiyo.

Wazo hilo likachukuliwa moja kwa moja na mwanzoni kutoka jina la Sunderland,kweli Simba ilikuwa ikiitwa Simba Mwekundu lakini baadaye ndipo ilipoandikishwa kama Simba Sports Club,jina alilolitoa hayati Karume kwa mdomo wake kabisa nami nikimsikia kwani mwaka 1971 nilikuwa mvulana wa shule ya msingi na sikuwa mdogo sana.Inasikitisha sana siku niliposoma mahali mdau mmoja wa Simba akisema jina hilo walilibuni wana Sunderland wenyewe baada ya Serikali kupiga marufuku majina ya vyama fulani vya nje.Hapana,huo ni upotoshaji wa dhahiri wa Historia,jina hilo lilitengenezwa kichwani mwa hayati Karume.Kama kweli Simba wenyewe waliliteua jina hilo kuwa lao badala ya Sunderland,basi tukubaliane kwamba uteuzi huo ulifanywa katika kurasmisha mapendekezo aliyoyatoa hayati Karume.

Kwa msingi ulio sahihi wa historia ya Yanga na Simba,hayati Karume anaweza kutajwa kuwa ndiye aliyezifanya klabu hizo ziwepo leo,ndiye aliyeshiriki moja kwa moja kuzipatia majengo wanayonufaika nayo leo na ndiye aliyeasisi jina la Simba Sports Club.Kama ilivyoelezwa,Simba ilianzishwa toka ubavuni mwa Yanga iliyoanzishwa kwa uasisi na ushawishi wa hayati Karume mwaka 1928 akiwa na umri wa miaka 23. Baadhi ya watu toka klabu hiyo moja walijitenga mwaka 1936 na kuanzisha klabu hii inayojulikana sasa kama Simba Sports Club.Ni kutokana na maelezo hayo ya kweli ya kihistoria ndipo unapoweza kumuweka hayati Abeid Aman Karume katikati ya uanzishwaji wa klabu zote za Yanga na Simba na unaweza pia kumuweka katikati ya mipango yake mikubwa ya maendeleo kama kumiliki majengo ambayo yanafaa kutumika kama vitega uchumi vya klabu hizo.

Ninamaliza kwa kutoa maombi manne.Kwanza,kwenye siku ya Karume Day ni vizuri tukimkumbuka Mwanamapinduzi huyo kwa kuwaeleza vijana makubwa aliyoifanyia nchi hii si kisiasa tu na kiuchumi bali pia kijamii kama nilivyofanya leo kuonyesha mchango wake kwa klabu za Yanga na Simba.Si vizuri watu kupumzika tu na kusema kuwa leo ni siku ya kumbukumbu ya tarehe aliyouwawa Karume,kwani kuuwawa kwa kiongozi wetu huyo kuna nini cha kutufanya tuitukuze siku hii? Mantiki ya kuifanya siku hii kuwa kuu ni kukumbushana kwa maandiko,kwa utangazaji na kwa makongamamo kuhusu mchango wa kiongozi wetu huyo kwa maendeleo yetu yakiwemo ya klabu za Yanga na Simba.

Pili,naomba jamii ya wapenda soka wa nchi hii iwe inaandaa mechi kubwa tu kwenye siku hii zenye sura ya Muungano wetu alioshiriki kuuasisi.Kunaweza kuwepo mechi ya kirafiki ya Kilimanjaro Stars na Zanzibar Heroes au timu mchanganyiko ya Dar es Salaam na timu mchanganyiko ya Zanzibar na Chakechake,au Simba na Malindi ama Yanga na Miembeni na kadhalika.

Tatu,uwanja wa kumbukumbu ya Karume wa Ilala Dar es Salaam,ambao ndiyo wenye historia kubwa ya soka ya nchi hii,urudishwe kuwa wa kutumika kimashindano badala ya kugeuzwa wa mazoezi mazoezi,vimechi vidogo vidogo na makao makuu ya TFF! Unapaswa urudishwe kutumika kimashindano kwa mechi kadhaa kwa kutengenezewa majukwa ya kukaa watazamaji,jambo ambalo ni rahisi sana kufanyika kwa kuhusisha taasisi za kibiashara na kuingia mkataba nao wa kutengeneza majukwa hayo kwa makubaliano maalum ikiwemo kutangazia biashara zao uwanjani hapo.

Wakati mwingine tuwe tunafikiria kujenga.Tutakuwaje wahitaji wa maendeleo kwa kusubiri kila kitu tujengewe? Tujenge majukwaa ya uwanja wa Kumbu kumbu ya Karume ili miaka ijayo kwenye ligi kuu timu za Manyema Rangers,JKT Ruvu,Moro United,Azam na African Lyon zenye makao yake Dar es Salaam kimashindano ziutumie uwanja huo kama wa nyumbani zinapocheza na timu nyingine zote isipokuwa Yanga na Simba kama Mtibwa Sugar walivyo na Manungu na Jamhuri. Naomba ifanywe hivyo ili kulifanya jina la uwanja huo lilingane na ukubwa na umaarufu wa mtu mwenye jina hilo.

La mwisho, naomba sana historia iandikwe vizuri na kwa upande wangu naomba historia iwekwe sawa kuhusu jinsi Yanga na Simba zilivyoanzishwa,zilivyopata majengo yao na jinsi Simba ilivyobadilika toka kuwa Sunderland hadi kuwa Simba.Nimeeleza hapa kila nilicho na uhakika nacho lakini wangapi wataniamini? Naomba Mwenyezi Mungu azidi kuitunza mahala pema peponi roho ya Sheikh Abeid Aman Karume.Amen.

Sunday 18 April 2010

IS IT FOR GOD'S SAKE TRUE THAT KISWAHILI HAKIPANDI KABISA TO SOME OF OUR FELLOW TANZANIANS?!!

By Ibrahim Mkamba

ONE Tanzanian of moderate fame who had lived abroad for less than three years was interviewed live in a certain Kiswahili local radio station when she was here in Tanzania.She was asked in Kiswahili,"hebu tueleze ni nini unachofanya huko unakoishi kwa sasa?".Her response was more in English than what it was supposed to be! "em, em, em un'jua kuli ziidi nin'shughlika na beauty pageant,as you know that is the work to which I am highly experienced ne kwe kweli I'm doing it well given that people there are more interested in that artistic work than the people here" She did that in English accent whenever she was uttering few Kiswahili words here and there in what was supposed to be a total Kiswahili interview!

Due to that,her host in that programme had to carry a burden of making translations for Kiswahili listeners who could not grasp much of what the artist was saying."yaani unajishughulisha na shughuli za urembo ulizo na uzoefu nazo na umesema kwamba kule unapata mafanikio kutokana na watu wengi wa huko kuipenda fani hii kuliko wa hapa.Unafikiri kwa nini fani hii hapa iko chini?" The host would translate tactifully and pose a question to the artist.

"Yeh,I think it is all because tradition and custom of these two communities differ....." She would respond a Kiswahili question completely in English! The drama went on like that up till when the host could stand that no more and asked the artist an embarrassing question; "Ina maana siku hizi Kiswahili hukiwezi kabisa?"

"Aaam no, not at all because Kiswahili is my language,siwezi kus'hau lugh'yangu but these days I find it difficult to speak Kiswahili continuously..." Again,more English than Kiswahili even in answering a question as to whether she was no longer capable of speaking Kiswahili!

This is just an example of many Tanzanians who pretend to be better in speaking English than Kiswahili,upon living out of our country in countries of English speaking citizens for a very short time,say,three years or less.This childish act and ushamba is quite nauseating.For example,that Kiswahili radio programme was a sheer nauseating as it was informally transformed into English one for stupidity of one Tanzanian in an endeavour to show her fellow Tanzanians that she was then more mzungu than African of Tanzania origin!

Those Tanzanians of calibre of the above written about artist have something wrong in their upstairs.Most of them have not lived in such countries as United Kingdom (UK)or United States of America (USA) longer than what has been done by a famous Tanzanian intellectual Professor of Communications and Public Policy, Nicholls Boas,of the University of Maryland,USA who has been there for some decades,lecturing the English speaking people and socially interacting with the English speaking people throughout that long period of time.

Even thus, not only is he fluent in Kiswahili but also his accent of that language is a Dar es Salaam one.He never mixes up Kiswahili with English when speaking the former languge.When giving lecture to Swahili people in English, he uses pronounciations which are understandable to them but when he imitates the Americans in giving some examples in his lectures,he speaks completely the way they do.I happen to know all those qualities of that Professor, who is a regular analyst in international Kiswahili radio programmes, such as the BBC London and Radio Deutch Welle Kiswahili Services, because I was once one of his students in a certain short course.

There are some more Tanzanians who live abroad for a number of years but have not pretended to have lost their fluency in Kiswahili because they are intelligent and wise.Also,I have an example of three people I came into contact with at the University of Dar es Salaam and one of them from Mzumbe High School,Morogoro.Those are Lawyers Anthony Charles Rutabanzibwa whom I knew from Mzumbe,Holo Hussein Makwaiya and Minister of Home Affairs,Lawrence (Law)Kego Masha.All those three lawyers were living abroad from their infancy and got their Primary and part or all of Secondary School education there but when coming to Tanzania,already grown ups,they started speaking good Kiswahili of which they have now had mastery as proved by good Kiswahili speeches of Honourable Masha.

How come then a person who is born here,gets all of his or her upbringings here,gets the whole of his or her education here in our primary schools of Kiswahili Medium of Instructions to banish Kiswahili after living abroad for only three years?Ujinga kabisa huu.

It is quite surprising to see some of the Waswahili treading on their language, the fame of which is going up and up worldwide as time goes by!Look here,such celebrated African personalities like the former President of Mozambique,Joachim Chissano,the former President of Zambia,Frederick Chiluba, the President of Uganda,Yoweri Museveni and the President of DRC,Joseph Kabila are very proud of being fluent in Kiswahili because they know that the language is the only African language which cuts across the whole of the continent.Also those big people and other wise Africans know that Kiswahili is now one of the biggest languages of the world.

Yes,the language cuts across the whole of Africa continent as now you will hardly find no person capable of speaking Kiswahili wherever you go in Africa.During this year's Africa Cup of Nations tournaments in Angola,BBC Swahili Service was interviewing in Kiswahili many African traders based in Angola,coming from different countries far from East Africa,such as Mali.

I remember a friend of mine Mr.Mancoba Qubecca (I am sorry,I may have miss-spelt his names the way most of us fail to pronounce them correctly due to the unique pronounciations of the same!),a South African whom I met at Tanzania School of Journalism (TSJ) in Dar es Salaam in 1987.That man who is the ANC spokesman was recently interviewed by BBC Kiswahili Service and he spoke Kiswahili very fluently,mixing up few English words only when he had no option other than doing that.He left Tanzania about 20 years ago but he has never pretended to have forgotten Kiswahili,the language he learned while he had already been an adult person.

It is very interesting that an Englishman,Sir Edward Twinning,the last but one British Governor to Tanganyika, when bidding farewell to the Tanganyikans before he left in mid 1950's he delivered a very good Kiswahili speech of farewell just like what was done by his wife in the same ocassion.They respected Kiswahili but some of us banish it.If they did not respect it,they would deliver their respective speeches in English with Kiswahili interpretation.

Few years ago,father of the English pressman captured in Iraqi warfield spoke through the BBC Kiswahili Service on how he was highly delighted after life of his son was spared.He did that right from London where he was living but in a very fluent Kiswahili which he said he learned when he was living in Tanzania from colonial era up to early 1970's.He has not lost his fluency of the language, his being far from Waswahili for a long time notwithstanding.

One of the pillars of the defunct Empire Bakuba of the late Pepe Kalle,one Dilu Dilumona,a vocalist and a composer,is very fluent in Kiswahili which he learned when he was here in Tanzania for a short time with Bana Ngenge Music Band in 1970's but our fellow Waswahili pretend to lose capability of speaking the language after very short stay out of Tanzania!

It is quite ridiculous that we made a big mockery to our fellow Tanzanian,famous local film star for failing to speak fluent English abroad while we laud and see her to be very special person the Tanzanian artist who says she is no longer fluent in Kiswahili! Tuache ujinga kwani siamini kabisa kwamba kuna Mtanzania anaweza kupoteza uwezo wake wa kuzungumza Kiswahili baada ya kuishi nje akiwa mkubwa na tayari akiwa ameshaijua lugha hiyo kubwa ya dunia.